MICHEZO NA BURUDANI
PATA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI KEMKEM MwangaTZ APELEKWA POLISI KWA KUFANANA NA LIONEL MESSI MAY 09, 2017 Mwanafunzi mmoja nchini Iran amelazimika kupelekwa katika kituo cha polisi mwishoni mwa wiki iliyopita kisa na mkasa! Kufanana kulikokithiri na Lionel Messi. Watu wengi katika mji wa Hamaden wamekuwa wakiomba kupiga picha na kijana huyo aitwaye Reza Parastesh, na hivyo kusababisha msongamano wa watu kila atakakokanyaga, hivyo polisi walilazimika kumhifadhi kwa muda ili kuondoa msongamano huo. Mkanganyiko huo ulianza miezi michache iliyopita wakati ba a wa kijana huyo aliyefanana mno na Messi alipompiga picha akiwa amevalia fulana ya timu ya Barcelona yenye namba kumi. Reza Parastesh, ana umri wa miaka ishirini na mitano kwa sasa, hivi karibuni alianzisha mtindo wa ukataji nywele na kupunguza ndevu zake mithili ya mshambuliaji huyo wa timu ya taifa ya Argentina .Reza Parastesh, kwa sasa amebatizwa jina 'Messi wa Ira...